
Kumekuwa na utata kuhusu Kambi ya Nigeria, yenye Mastaa wakubwa kina Yakubu Ayegbeni , Obafemi Martens, Kanu na wengineo, huku kukiibuka minong’ono kuwa kuna mtafuruku mkubwa kambini lakini Kanu amezikanusha vikali taarifa hizo.
Msumbiji v Benin
Mara baada ya patashika ya Misri v Nigeria, Uwanjani hapo hapo Ombaka, Msumbiji wataingia kupambana na Benin katika mechi ya pili ya Kundi C itakayoanza saa 3 na nusu usiku saa za bongo.
Kocha wa Msumbiji kutoka Uholanza, Mart Nooij, amesema Kikosi chake kipo imara na wanajiamini.
Nao Benin watamtegemea sana Straika wao Razak Omotoyossi anaechezea FC Metz ya huko Ufaransa.
No comments:
Post a Comment