Tuesday 12 January 2010

Misri v Nigeria
Mechi hii ya Vigogo wa Afrika itachezwa leo saa 1 usiku, saa za bongo, Uwanja wa Taifa wa Ombaka Mjini Benguela, Angola.
Hii ni mechi ya Kundi C na Mabingwa Watetezi wa Afrika, Misri, wataanza utetezi wa taji lao dhidi ya Timu ngumu Nigeria huku wakiwa na upungufu mkubwa kwenye Kikosi chao kwa kuwakosa Mastaa Mido, Amr Zaki na Mohammed Aboutrika ambao wameachwa kwa vile ni majeruhi.
Kumekuwa na utata kuhusu Kambi ya Nigeria, yenye Mastaa wakubwa kina Yakubu Ayegbeni , Obafemi Martens, Kanu na wengineo, huku kukiibuka minong’ono kuwa kuna mtafuruku mkubwa kambini lakini Kanu amezikanusha vikali taarifa hizo.
Msumbiji v Benin
Mara baada ya patashika ya Misri v Nigeria, Uwanjani hapo hapo Ombaka, Msumbiji wataingia kupambana na Benin katika mechi ya pili ya Kundi C itakayoanza saa 3 na nusu usiku saa za bongo.
Kocha wa Msumbiji kutoka Uholanza, Mart Nooij, amesema Kikosi chake kipo imara na wanajiamini.
Nao Benin watamtegemea sana Straika wao Razak Omotoyossi anaechezea FC Metz ya huko Ufaransa.

No comments:

Powered By Blogger