Monday 11 January 2010

NGOMA NGUMU: Ivory Coast 0 Burkina Faso 0
Mjini Cabinda, Mji uliokumbwa na msiba mkubwa kufuatia vifo vilivyotokea baada ya Basi la Timu ya Togo kupigwa risasi na Waasi, leo mechi ya kwanza ya Kundi B kati ya Ivory Coast na Burkina Faso ilichezwa na hakuna mbabe aliepatikana baada ya kutoka sare ya 0-0.
Mechi nyingine ya Kundi hili iliyotakiwa kuchezwa kati ya Ghana na Togo haifanyiki kwa vile Togo wamejitoa na kurudi kwao kwa mazishi ya Kocha wao Msaidizi na Afisa Habari wa Timu.
Ivory Coast walistahili kushinda mechi hii kwa vile waliitawala na kuwabana Burkina Faso nusu uwanja lakini Kikosi chao kilichojaa Mastaa kina Drogba, Kone, Yaya Toure, Kolo Toure, Eboue, Kalou na Dindane kilishindwa kupata hata kigoli cha babu.
Sasa Ivory Coast wana kimbembe kikubwa hapo Januari 15 watakapovaana na Timu ngumu Ghana.
MECHI ZA KESHO Januari 12: [saa za bongo]
[KUNDI C Mjini Benguela]
Egypt v Nigeria [saa 1 usiku]
Mozambique v Benin [saa 3 na nusu usiku]

No comments:

Powered By Blogger