Friday 15 January 2010

Redknapp kwa Pilato!!!
• Ashitakiwa kwa kukwepa kodi!!
Aliekuwa Meneja wa Portsmouth, Harry Redknapp, ambae sasa ni Meneja Tottenham, atasimama kizimbani Februari 11 kujibu mashitaka mawili ya kudanganya umma na kutolipa kodi makosa yanayodaiwa kutendeka kati ya Aprili 1, 2002 na Novemba 28, 2007 alipokuwa Meneja wa Portsmouth.
Harry Redknapp alikuwa Meneja wa Portsmouth kwa vipindi viwili, cha kwanza kikiwa kati ya Machi 2002 hadi Novemba 2004 na cha pili kati ya Desemba 2005 hadi Oktoba 2008.
Mashitaka hayo yanafuatia uchunguzi wa Polisi na Mamlaka za Kodi uliodumu miezi 26 na inadaiwa unahusiana na malipo ya jumla ya Pauni 183,000 kutoka kwa aliekuwa Mwenyekiti wa Portsmouth Milan Mandaric kupitia akaunti ya Benki huko Monaco na hivyo kukwepa ulipaji kodi.
Redknapp ameshitakiwa pamoja na Mandaric.

No comments:

Powered By Blogger