Thursday 14 January 2010

Mali v Algeria
[saa 1 usiku, bongo taimu]
Leo Uwanjani Novemba 11 huko Luanda, Angola, Algeria watakuwa wakipagania kubaki kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuchapwa 3-0 na Malawi katika mechi yao ya kwanza ya Kundi A watakapocheza na Mali iliyotoka sare na Wenyeji Angola kwa bao 4-4 baada ya kuwa nyuma 4-0 huku zikiwa zimebaki dakika 12 mchezo kumalizika.
Mali leo inategemewa kumchezesha Kiungo wa Juventus Mohamed Sissoko ambae hakucheza mechi ya kwanza kwa sababu ya maumivu lakini Kocha wa Mali Stephen Keshi hakuthibitisha hilo.
Algeria, waliopigwa 3-0 na Malawi, ilibidi waiombe Nchi yao radhi kwa kipigo hicho na Mchezaji wao wa Rangers ya Scotland, Beki Madjid Bougherra ameahidi maajabu leo.
Angola v Malawi
[saa 3 na nusu, bongo taimu]
Mara baada ya Mechi ya leo kati ya Mali na Algeria kwisha ndani ya Uwanja wa Novemba 11 huko Luanda, Angola, Wenyeji Angola watajimwaga humo kuivaa Malawi na Kocha wao Manuel Jose ameahidi mchezo tofauti na ule walioiruhusu Mali kufunga bao 4 katika dakika 12 za mwisho.
Nae Kocha wa Malawi Kinnah Phiri amesema Timu yao haina wasiwasi na watatulia uwanjani.
Adebayor hajui lini ataweza kucheza!
Straika wa Manchester City ambae ni Nahodha wa Togo, Emmanuel Adebayor, alienusurika baada ya Basi la Timu ya Togo kushambuliwa kwa risasi likiwa njiani kutoka Congo na kuelekea Mjini Cabinda huko Angola na kuwaua Kocha Msaidi na Afisa Habari wa Togo na pia Dereva wa Basi hilo, amesema hana uhakika lini ataweza kucheza tena Soka baada ya kupata mstuko mkubwa.
Meneja wa Manchester City Roberto Mancini amesema wao watampa muda wowote anaotaka ili kupumzika na kujijenga upya kifikra.
Mpaka wakati huu, Adebayor bado yuko kwao Lome, Togo.
Barca nje Copa del Rey!!
Licha ya kuifunga Sevilla 1-0 hapo jana, Mabingwa Watetezi wa Copa del Rey, FC Barcelona, wametupwa nje ya Kombe hilo kwa sheria ya goli la ugenini kwa vile Sevilla iliifunga Barca 2-1 huko Nou Camp nyumbani kwa Barcelona.

No comments:

Powered By Blogger