Friday 15 January 2010

Ivory Coast yatinga Raundi ya Pili!!
• Ivory Coast 3 Ghana 1
Ivory Coast ndio Timu ya kwanza kuingia Raundi ya Pili ya Kombe la Afrika baada ya kuifunga Ghana iliyochezesha Vijana wadogo wengi mabao 3-1.
Mpaka mapumziko, Ivory Coast ilikuwa mbele ka bao 1-0 Mfungaji akiwa Gervinho baada ya krosi tamu ya Salomon Kalou.
Kipindi cha pili kilianza kwa Ghana kumuingiza Michael Essien na kwa Ivory Coast haikuchukua muda pale Emmanuel Eboue alipowashwa Kadi Nyekundu na Refa Damon baada ya kucheza rafu mbaya kwa Opoku Agyemang.
Lakini, Ivory Coast hawakutetereka na Siaka Tiene akawapatia bao la pili kwa frikiki nzuri sana na Didier Drogba akafunga bao la 3 kwa kichwa kufuatia krosi ya Kader Keita.
Ghana walipata bao lao moja kwa njia ya penalti waliyopewa baada ya Soulemane Bamba kumwangusha Asamoah Gyan na Gyan akafunga mwenyewe hiyo penalti.
Sasa Ghana inabidi waifunge Burkina Faso katika mechi yao ya mwisho ili kusonga Raundi ya Pili na wakitoka suluhu Burkina Faso watafuzu na Ghana nje.
Mechi hiyo itachezwa Jumanne Mjini Luanda, Angola badala ya Cabinda ambako Kundi hili lilicheza mechi zake.
Vikosi vilivyoanza:
Ivory Coast: 1-Boubacar Barry; 17-Siaka Tiene, 4-Kolo Toure, 21-Emmanuel Eboue, 22-Soulemane Bamba; 5-Didier Zokora, 6-Yaya Toure, 9-Cheik Tiote, 8-Salomon Kalou; 10-Gervinho, 11-Didier Drogba.
Ghana: 22-Richard Kingson; 18-Eric Addo, 7-Samuel Inkoom, 15-Isaac Vorsah, 11-Moussa Narry; 19-Emmanuel Agyemang-Badu, 9-Opoku Agyemang, 13-Dede Ayew, 17-Rahim Ayew, 14-Mathew Amoah, 10-Kwadwo Asamoah.
Refa: Jerome Damon (South Africa)
MECHI ZA Januari 16:

[saa za bongo]
[KUNDI C]
Nigeria v Benin [saa 1 usiku]
Egypt v Mozambique [saa 3 na nusu usiku]

No comments:

Powered By Blogger