Thursday 14 January 2010

Fergie: “Safari ya Qatar ni ya mafanikio!!”
Manchester United leo wanarudi kwao England baada ya ziara ya mazoezi ya siku 4 huko Doha, Qatar ambako walikuwa wageni wa Chuo cha Aspire.
Ziara hiyo pia ilikuwa kulikimbia baridi na barafu zilizoiandama Uingereza na kufanya mazoezi ya Timu yawe ni kwenye Jimu tu kwani nje hakuchezeki.
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, ameisifia ziara hiyo na kudai itaisaidia sana kwenye matayarisho yao ya mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu huko Old Trafford dhidi ya Burnley.
Ferguson amesema: “Ni mafanikio kuwa Qatar! Chuo cha Aspire ni cha kisasa kabisa na kinaendeshwa kitaalam na vizuri sana!”
Ferguson alimalizia kwa kusema kuwa ziara hiyo imefungua milango kwa safari nyingine na watadumisha urafiki wao na Aspire.
Jana, mazoezi ya Man U yalikuwa wazi kwa Washabiki kwenda kuyatazama na watu wengi walifurika kwenda kuwaona Mabingwa hao hapo Chuono Aspire.
Chuo cha Aspire hukuza vipaji vya Vijana toka kila pembe ya Dunia na huendeshwa na Wataalam wa hali ya juu.

No comments:

Powered By Blogger