Saturday 16 January 2010

LIGI KUU: Everton 2 Man City 0
Walisema leo ndio mtihani wa kweli kwa Meneja wa Manchester City, Roberto Mancini, ambae tangu achukue hatamu ameshinda mechi kadhaa za Ligi Kuu lakini Wadau walidai alicheza na Timu ‘dhaifu’ kama Stoke na Wolves na leo kukutana na Everton ndio kigingi chake.
Na kweli, ndani ya Goodison Park, Everton walifanya kweli nyumbani kwao na kumpa Mancini na Man City yake somo kali la kandanda pale walipoifunga bao 2-0 na pengine mabao hayo ni salama yao kwani Everton walitawala kabisa na kukosa lundo la magoli.
Wafungaji wa Everton walikuwa Steven Pienaar dakika ya 36 kwa frikiki murua na Saha dakika ya 45 kwa penalti baada ya Micah Richards kumvuta jezi Saha.
Katika mechi hii Robinho alianza benchi lakini akaangizwa dakika ya 8 tu ya mchezo baada ya Santa Cruz kuumia na cha kushangaza ni kule kutolewa kwa Robinho kipindi cha pili na kuingizwa Shaun Wright-Philipps kitendo ambacho inaelekea kilimkera Robinho kwani alipotolewa tu Robinho hakwenda kukaa benchi bali alitoka na kwenda moja kwa moja kwenye vyumba vya kubadilisha jezi.
Pengine huu ndio mwanzo wa mwisho kwa Robinho hapo Man City.
Vikosi vilivyoanza:
Everton: Howard, Neville, Heitinga, Distin, Baines, Donovan, Fellaini, Pienaar, Bilyaletdinov, Cahill, Saha.
Akiba: Nash, Vaughan, Forshaw, Coleman, Duffy, Baxter, Mustafi.
Man City: Given, Zabaleta, Richards, Kompany, Garrido, Petrov, De Jong, Barry, Bellamy, Tevez, Santa Cruz.
Akiba: Taylor, Onuoha, Sylvinho, Wright-Phillips, Robinho, Mwaruwari, Boyata.
Refa: Andre Marriner

No comments:

Powered By Blogger