Tuesday 12 January 2010

Misri waibutua Nigeria!!!
Mabingwa Watetezi wa Afrika, Misri, leo wameanza kampeni yao ya kutetea taji lao murua baada ya kuibamiza Nigeria mabao 3-1 Uwanja wa Taifa wa Ombaka Benguela, Angola katika mechi ya Kundi C.
Ni Nigeria walioanza kwa kufunga bao zuri la Straika wa Hoffenheim ya Ujerumani, Chinedu Obasi, aliefumua shuti ambalo liliuparaza mkono wa Kipa hodari wa Misri El Hadari na hiyo ilikuwa ni dakika ya 12.
Mshambuliaji wa Misri Emad Moteab alisawazisha dakika ya 33 na Timu zilienda mapumziko zikiwa sare 1-1.
Kipindi cha pili, Misri iliongeza kasi na kupata bao mbili kupitia Nahodha Ahmed Hassan dakika ya 53 na Mchezaji alietoka benchi Gedo dakika ya 88.
Mechi zijazo za Timu hizi ni Januari 16 na ni Misri v Msumbiji na Nigeria v Benin.
Muda mfupi ujao, hapo hapo Ombaka, mechi ya pili ya Kundi C kati ya Msumbiji na Benin itaanza.
VIKOSI:
Egypt: El Hadari, Fathallah, Said, Moawad, Gomaa, Fathi, Abd Rabou, Ghaly, Hassan, Zidan, Moteab.
Akiba: Abdoul-Saoud, El Mohamady, Salem, El Sakka, Eid, Tawfik, Gedo, Wahid,
Shikabala, Abdelshafy, Raouf, Hamdy.
Nigeria: Enyeama, Yobo, Taiwo, Nwaneri, Mohammed, Mikel, Yussuf, Uche, Etuhu, Obasi Ogbuke, Yakubu.
Akiba: Ejide, Apam, Echiejile, Kaita, Kanu, Martins, Obinna, Odemwingie, Odiah, Olofinjana, Shittu, Aiyenugbu
MECHI ZA KESHO Januari 13: [saa za bongo]
[KUNDI D Mjini Lubango]
Cameroun v Gabon [saa 1 usiku]
Zambia v Tunisia [saa 3 na nusu usiku]

No comments:

Powered By Blogger