Thursday 14 January 2010

KOMBE la Afrika: Angola 2 Malawi 0
• Angola juu Kundi A!!
Watoto wa nyumbani, Angola, leo wamewapa furaha kubwa Raia wao baada ya kuilaza Malawi 2-0 katika mechi ya Kundi A la Kombe la Mataifa ya Afrika iliyochezwa leo Mjini Luanda, Angola.
Flavio ndio alieungua ufungaji kwa kufunga bao la kwanza na Manucho akapachika bao lapili.
Kwa ushindi huo, Angola ni vinara wa Kundi A na wana pointi 4, wanafuata Malawi pointi 3, kisha Algeria pointi 3 na Mali pointi 1.
Mechi za mwisho Kundi hili ni Angola v Algeria na Mali v Malawi.
MECHI ZA Januari 15: [saa za Bongo]
[KUNDI B]
Burkina Faso v Togo [hamna Togo wamejitoa]]
Ivory Coast v Ghana [saa 3 na nusu usiku]
KOMBE la AFRIKA: Mali 0 Algeria 1
• Kundi A linazidi kuwa hekaheka!!!
Algeria leo wameibuka kidedea baada ya kipigo cha mechi ya kwanza walipowashwa 3-0 na Malawi na leo kuwafunga Mali waliotoka suluhu na Wenyeji Angola 4-4 kwa bao 1-0.
Bao la dakika ya 43 la Haliche ndilo limefufua matumaini ya Algeria.
Sasa baada ya mechi mbili kwa Timu hizi, Algeria wana pointi 3 na Mali pointi moja na Timu hizi zitamaliza mechi zake kwa kucheza Januari 18 Algeria watakapocheza na Angola na Mali watakutana na Malawi.
Mechi inayofuata leo ya Kundi A ni Angola v Malawi.
Pigo Kuu kwa Liverpool!!!
Licha ya kutandikwa 2-1 na “Timu ndogo” Reading hapo jana mbele ya Mashabiki wake nyumbani Anfield na hivyo kutupwa nje ya Kombe la FA, imethibitika kuwa Liverpool itawakosa Mastaa wake watatu kwa wiki kadhaa baada ya wote kuumizwa katika kipigo hicho cha jana.
Fernando Torres, alieshindwa kumaliza mechi ya jana baada ya kutolewa nje kwa maumivu katika muda usiozidi nusu kwenye mechi hiyo ya jana na Reading, inabidi afanyiwe operesheni goti lake la kulia na atakuwa nje kwa muda usiopungua wiki 6.
Nahodha Steven Gerrard yeye alidumu hadi mapumziko kwenye mechi hiyo na imethibitika ana tatizo la musuli na atakuwa nje hadi wiki mbili.
Mchezaji mwingine nyota Msimu huu, Yossi Benayoun, yeye amevunjika mbavu na atakuwa nje hadi miezi miwili.
Hayo ni mapigo makubwa sana kwa Liverpool na yanamzidishia presha kubwa Meneja Rafa Benitez huku zikiibuka tena kelele afukuzwe toka kwa baadhi ya Mashabiki wakidai kutolewa nje kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE, FA Cup, Carling Cup na kusuasua kwenye Ligi ni aibu kubwa kwao.
Leo ni Nusu Fainali ya kwanza Carling Cup
Blackburn Rovers na Aston Villa leo zinapambana kwenye mzunguko wa kwanza wa Nusu Fainali ya Kombe la Carling huko Ewood Park nyumbani kwa Blackburn baada ya mechi hii kuahirishwa wiki iliyopita kutokana na barafu.
Mechi ya pili ya marudiano ya Nusu Fainali kati ya Aston Villa v Blackburn itachezwa Villa Park tarehe 20 Januari.
Nusu Fainali nyingine ni Manchester City v Manchester United na itachezwa Januari 19 huko City of Manchester Stadium na marudio ni Januari 27 huko Old Trafford.

No comments:

Powered By Blogger