Tuesday 12 January 2010

Man City yaikwaa nafasi ya 4 Ligi Kuu!!
• Man City 4 Blackburn 1
Magoli matatu yaliyofungwa na Mchezaji anaeng’ara sana kwa sasa hivi, Carlos Tevez, na moja la Beki Micah Richards, yamewapa ushindi mnono Manchester City Uwanjani kwao City of Manchester baada ya kuwatwanga Blackburn Rovers mabao 4-1 kwenye mechi ya Ligi Kuu hapo jana usiku na hivyo kuifanya Man City iikwae nafasi ya 4 kwenye Ligi.
Carlos Tevez alifunga mabao yake matatu dakika za 7, 49 na 90. Richards alipachika la kwake dakika ya 39.
Goli pekee la Blackburn lilifungwa na Pedersen dakika ya 71.
Van der Sar arudi mazoezini Man U!!
Kipa Nambari Wani wa Manchester United Edwin Van der Sar hapo sasa ameanza mazoezi na Timu yake tangu aenda kumuuguza Mkewe mwezi uliopita baada ya kupewa likizo ya dharura na Man U kufuatia kuugua ghafla kwa Mkewe huko kwao Uholanzi.
Kabla ya kupata dharura hiyo, Van der Sar alikuwa hajaidakia Man U tangu Novemba 21 walipoifunga Everton 3-0 na akaumia goti kwenye mechi hiyo.
Van der Sar yupo kwenye Kikosi cha Manchester United kilichotua Doha, Qatar hapo juzi kwa mazoezi ya siku 4.
Kipa wa Akiba Tomasz Kuszczak ndie alikuwa akiidakia Man U kwa kipindi chote Van der Sar alichokosekana.

No comments:

Powered By Blogger