Monday 11 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Togo warudi kwao kwa mazishi, maombolezo siku 3!!
  • Wataka kurudi tena Angola wakimaliza msiba, CAF yagoma!!!
Wakati mechi ya ufunguzi kati ya Wenyeji Angola na Mali ikianza huko Luanda Mji mkuu wa Angola hapo jana usiku, Timu ya Togo ilikuwa njiani kwenda Uwanja wa Ndege wa Cabinda, Angola ili kupanda Ndege waliyoletewa na Rais wa Nchi yao, Faure Gnassingbe, ili kurudi kwao huku wakiibeba miili ya wenzao wawili waliouwa kwenye shambulizi la la risasi wakiwa kwenye Basi hapo majuzi mara tu baada ya kuingia Angola wakitokea Congo.
Kikosi hicho cha Togo kiliamriwa kurudi Togo kwa mazishi na maombolezo ya siku 3 yaliyotangazwa na Nchi yao.
Hata hivyo, Waziri wa Michezo wa Togo, Christophe Tchao, alisema wameiomba CAF kurekebisha Ratiba ili waweze kurudi Angola baada ya mazishi na maombolezo lakini CAF inaelekea haitakubali ombi hilo.
Togo walikuwa leo wacheze na Ghana kwenye mechi ya Kundi B.
MECHI ZA LEO: Jumatatu Januari 11 [saa za bongo]
KUNDI A [Luanda]
Malawi v Algeria [saa 10 dk 45 jioni]
KUNDI B [Cabinda]
Ivory Coast v Burkina Faso [saa 1 usiku]
Ghana v Togo [Hamna mechi, Togo imejitoa]
Manchester United ndani ya Doha, Qatar!!

Kikosi kamili cha Mabingwa wa England Manchester United jana jioni kilitua Doha, Qatar ili kufanya mazoezi ya siku 4 wakiwa wageni wa Kituo cha Mafunzo ya Michezo cha Aspire ambacho ni spesheli kwa kukuza vipaji vya Vijana toka kila pembe ya Dunia.
Pichani ni Wachezaji wa Man U wakishuka toka kwenye Ndege Uwanja wa Kimataifa wa Doha [Picha ni toka Gulf Times, Qatar].
Manchester United wamelazimika kuja Doha ili kuikwepa hali ya hewa ya baridi kali na barafu nyingi iliyoikumba Uingereza ambayo imesababisha Michezo mingi kutochezeka na mazoezi kutofanyika kwenye Viwanja vya nje na hivyo kulazimisha Timu kufanya mazoezi kwenye Jimu tu.
Mabingwa hao kwa sasa wako nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu wakiwa pointi moja nyuma ya Chelsea na pia wapo Nusu Fainali ya Carling Cup na watacheza na Mahasimu wao wakubwa Manchester City wiki ijayo.
Vilevile, mwezi ujao watamenyena na AC Milan katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Mechi ambazo zinawakabili Man U hivi karibuni ni:
-Jumamosi, Januari 16: LIGI KUU: Man U v Burnley
-Jumanne, Januari 19: CARLING CUP: Man City v Man U
-Jumamosi, Januari 23: LIGI KUU: Man U v Hull
-Jumatano, Januari 27: CARLING CUP: Man U v Man City
-Jumamosi, Januari 31: LIGI KUU: Arsenal v Man U

No comments:

Powered By Blogger