Saturday 16 January 2010

LIGI KUU England: Portsmouth v Birmingham yaenda na maji!
Mechi ya Ligi Kuu kati ya Portsmouth na Birmingham iliyokuwa ichezwe leo saa 12 saa za bongo imefutwa baada ya Uwanja wa Fratton Park, nyumbani kwa Portsmouth, kujaa maji.
Mechi hii itapangiwa tarehe nyingine hapo baadae.
KOMBE LA AFRIKA: Leo Nigeria v Benin na Misri v Msumbiji
Mjini Benguela, Angola, Uwanja wa Taifa wa Ombaka, leo kutakuwepo na mechi mbili za Kundi C zikiwa ni mechi za pili kwa kila Timu.
Leo lazima Nigeria washinde baada ya kufungwa mechi ya kwanza na Misri mabao 3-1.
Benin walitoka suluhu 2-2 na Msumbiji katika mechi ya kwanza.
Ushindi kwa Misri utawaingiza Raundi ya Pili baada ya kushinda mechi ya kwanza 3-1 dhidi ya Nigeria.
Mechi za mwisho kwa Kundi hili ni Benin v Misri na Nigeria v Msumbiji.
Zaki njiani kurudi England!!
Amr Zaki huenda akarudi tena kucheza Ligi Kuu England safari hii na Klabu ya Hull City endapo mipango ya kwenda huko kwa mkopo itakamilika.
Amr Zaki ni Mchezaji wa Zamalek ya Misri na Msimu uliokwisha alikuwa na Wigan kwa mkopo na aliifungia Klabu hiyo mabao 11 lakini akakorofishana na Meneja wa Wigan wa wakati huo Steve Bruce na hivyo akakosa Mkataba wa kudumu hapo Wigan.
Zaki, miaka 26, hayupo kwenye Kikosi cha Misri kilichopo Angola kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kuwa ni majeruhi.
Owen kupata namba Man U!!!
Sir Alex Ferguson amemhakikishia Michael Owen kuwa mechi zijazo atakuwa anachezeshwa mara nyingi kupita siku za nyuma.
Ferguson amesema kutokucheza mara kwa mara kwa Owen ni tatizo la mbinu na mikakati kwenye fomesheni ya Man U na hasa kwa vile staili ya uchezaji ya Rooney na Owen inawafanya wao kuona ugumu wa kuwapanga kucheza pamoja.
Ferguson ametamka: “Owen inabidi apate mechi na hilo tunalitafutia ufumbuzi! Rooney hawezi kucheza kila mechi, inabidi apumzike na tutabadili mfumo wetu na
Owen atacheza tu!”
Pia, kuibuka kwa taarifa kuwa Dimitar Berbatov anauguza goti ambalo atafanyiwa operesheni mwishoni mwa Msimu na hivyo kumfanya apunguziwe mechi za kucheza, bila shaka kutaongeza nafasi kwa Owen kucheza.
Babel nje Kikosi cha Liverpool cha leo na Stoke!!
Inaelekea kibarua cha Ryan Babel huko Liverpool kinafikia ukingoni baada ya Winga huyo kutoka Uholanzi kutupwa nje ya Kikosi cha Liverpool kitakachocheza LigI Kuu leo na Stoke City licha ya Liverpool kutokuwa na Mafowadi wa kutosha kufuatia kuumia kwa Torres, Gerrard, Benayoun na kuuzwa kwa Voronin kwa Dynamo Moscow.
Hivi karibuni, Babel aliwahi kutangaza ni bora ahame Liverpool kwa vile hana namba ya kudumu na bora aende Timu ambayo atakuwa na namba ili aboreshe nafasi yake ya kuitwa Kikosi cha Uholanzi kitakachokwenda Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia mwezi Juni.

No comments:

Powered By Blogger