Monday 11 January 2010

LIGI KUU England leo: Manchester City v Blackburn Rovers
Manchester City leo watawakaribisha Blackburn Rovers Uwanjani kwao City of Manchester kwenye mechi pekee ya Ligi Kuu ambayo Mastafu wa Man City hapo uwanjani imebidi wafanye kazi ya ziada kuondoa barafu na kusafisha ili kuinusuru mechi hiyo isiahirishwe kama ilivyofanyika kwa mechi nyingi wikiendi hii iliyopita.
Ushindi kwa Man City leo utawafanya wawapiku Tottenham na kushika nafasi ya 4 kwenye msimamo wa Ligi na pia kuendeleza wimbi lao la ushindi la mechi 4 sasa huku Mchezaji wao Carlos Tevez akifunga kila mechi hivi karibuni na kumfanya apewe Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu kwa mwezi Desemba.
Patrick Vieira, Mchezaji mpya wa Man City waliemchukua kutoka Inter Milan kwa mkopo wa miezi 6, leo atashindwa kucheza mechi yake ya kwanza kwa vile ana maumivu ya musuli.
Vilevile, Man City itawakosa kina Shaun Wright-Phillips, Joleon Lescott, Nedum Onuoha na Stephen Ireland kwa kuwa wote ni majeruhi.
Pia, Kolo Toure na Emmanuel Adebayor hawatakuwemo kwa vile wako kwenye Timu zao za Taifa kwa ajili ya Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika huko Angola ingawa Adebayor sasa amerudi kwao Togo baada ya Timu hiyo kupata msiba mkubwa huko Angola.
Blackburn itawakosa Vince Grella ambae ni majeruhi na El-Hadji Diouf ambae amefungiwa baada ya kutwangwa Kadi Nyekundu katika mechi ilyopita ya Kombe la FA Blackburn waliyofungwa na Aston Villa.
VIKOSI VINATEMEGEWA KUWA:
Man City: Given, Zabaleta, Boyata, Kompany, Sylvinho, Wright-Phillips, De Jong, Barry, Petrov, Bellamy, Tevez.
Blackburn: Robinson, Chimbonda, Nelsen, Samba, Givet, Emerton, Andrews, N'Zonzi, Pedersen, McCarthy, Roberts.

No comments:

Powered By Blogger