Sunday 10 January 2010

SAKATA LA TOGO KOMBE LA AFRIKA:
  • Adebayor: “Tunarudi nyumbani!”
Nahodha wa Timu ya Togo, Emmaneuel Adebayor, amethibitisha Togo inarudi kwao baada ya kuamrishwa na Serikali yao kufuatia amri ya Waziri Mkuu Gilbrert Houngbo licha ya Wachezaji kukubaliana kwa kauli moja kuendelea kucheza Kombe la Afrika ili kuwaenzi wenzao waliouawa.
Basi lililokuwa likiwasafirisha Wachezaji wa Togo kutoka Congo lilishambuliwa kwa risasi mara ya baada ya kuingia jimboni Cabinda Nchini Angola na Dereva wake akauawa pamoja na Kocha Msaidizi na Afisa Habari wa Togo.
Shambulio hilo linasemekana imefanywa na Waasi wa Cabinda wanaopigania uhuru wa Jimbo hilo tajiri kwa mafuta.
Wachezaji wengine wawili walijeruhiwa vibaya na ilibidi wafanyiwe operesheni.
Adebayor pia amethibitisha kuwa Rais wa Togo Faure Gnassingbe ametuma Ndege yake ili kukisafirisha Kikosi cha Togo toka Cabinda hadi kwao Togo.
Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika yataanza rasmi leo usiku saa 4, saa za bongo, kwa pambano kati ya Wenyeji Angola na Mali litakalofanyika Mji Mkuu wa Angola, Luanda.

No comments:

Powered By Blogger