Monday 11 January 2010

Angola 4 Mali 4
Katika mechi ya ufunguzi ya Kombe la Mataifa ya Afrika huko Luanda, Angola, Wenyeji Angola na Mali walitoka sare 4-4
Angola itabidi wajilaumu wenyewe kwani walikuwa mbele kwa bao 4-0 lakini Mali wakarudisha bao zote.
Mpaka mapumziko Angola walikuwa mbele kwa bao 2-0 zilizofungwa na Flavio anaechezea Al Ahli ya Misri kwenye dakika ya 37 na 42.
Kipindi cha pili Angola wakaongeza bao nyingine mbili zote zikiwa za penalti Wafungaji wakiwa Gilberto, anaechezea Al Ahli kama Flavio, na Manucho, Mchezaji wa zamani wa Manchester United ambae sasa yuko Spain.
Mali walipata bao lao la kwanza dakika ya 78 ambalo alifunga Seydou Keita na Freddy Kanoute akafunga la pili dakika ya 87.
Bao la tatu la Mali lilifungwa tena na Seydou Keita dakika ya 89 na Mali wakasawazisha dakika ya 93 kupitia Mustapha Yatabare.
Mechi inayofuata kwa Kundi hili A ni kesho kati ya Algeria na Malawi na kisha Januari 14 Angola v Malawi na Mali v Algeria.
VIKOSI:
Angola: Fernandes, Mabina, Kali, Rui Marques, Stelvio, Xara, Dede, Zuela, Gilberto, Flavio, Manucho.
Mali: Sidibe, Diamountene, Berthe, Tamboura, Soumare, Diarra, Traore, Traore, Bagayoko, Maiga, Kanoute
MECHI ZA KESHO Januari 11:
[KUNDI A]
Malawi v Algeria
[KUNDI B]
Ivory Coast v Burkina Faso
Ghana v Togo [Togo imejitoa]

No comments:

Powered By Blogger