Saturday 16 January 2010

LIGI KUU: Ni mvua kubwa Darajani- Chelsea 7 S'land 2; Man U 3 Burnley 0; Spurs wabanwa mbavu!!!
Huko Stamford Bridge, Chelsea waliangusha kipigo kikubwa walipoibamiza Sunderland mabao 7-2.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Anelka, bao 2, Lampard, bao 2, na Ashley Cole, Malouda na Ballack bao moja kila mmoja.
Mabao ya Sunderland yalifungwa na Zenden na Darren Bent.
Mpaka mapumziko, Chelsea walikuwa mbele kwa bao 4.
Huko Old Trafford, baada ya kuwa suluhu 0-0 hadi mapumziko, Manchester United walishusha kipigo cha bao 3 kipindi cha pili.
Mabao ya Man U yalifungwa na Rooney, Berbatov na Diouf.
Mchezaji Mame Biram Diouf aliingizwa kipindi cha pili na hii ni mechi yake ya pili kuingizwa lakini ni ya kwanza kwa Uwanja wa Old Trafford na aliwainua Mashabiki wa Man U pale alipofunga bao tamu dakika ya 90.
Huko White Hart Lane, Tottenham ililazimishwa sare ya 0-0 na Hull City.
Nao Wolves walilambwa 2-0 na Wigan wakiwa nyumbani kwao kwa mabao ya kipindi cha pili yaliyofungwa na McCarthy na N'Zogbia.
Wachezaji Stearman wa Wolves na Thomas wa Wigan walitolewa nje kwa nyakati tofauti baada ya kupewa Kadi Nyekundu.
MATOKEO KAMILI:
Stoke 1 v Liverpool 1
Chelsea 7 v Sunderland 2
Man United 3 v Burnley 0
Portsmouth v Birmingham [IMEAHIRISHWA]
Tottenham 0 v Hull City 0
Wolves 0 v Wigan 2
[INAANZA saa 2 na nusu usiku]
Everton v Man City
MECHI ZA KESHO Jumapili, 17 Januari 2010
[saa 10 na nusu jioni]
Aston Villa v West Ham
[saa 12 jioni]
Blackburn v Fulham
[saa 1 usiku]
Bolton v Arsenal

No comments:

Powered By Blogger