Monday 14 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Holland 2 Denmark 0
Huko Soccer City, Soweto, leo Holland imeanza vyema kampeni zake za Kombe la Dunia walipoichapa Timu ngumu Denmark kwa bao 2-0.
Hadi mapumziko mabao yalikuwa 0-0.
Holland walipata bao lao la kwanza dakika ya 46 baada ya krosi ya Van Persie kumkuta Difenda wa Denmark Poulsen ambae badala ya kuokoa alipiga kichwa kilichomgonga mwenzake Agger na kutinga wavuni.
Dirk Kuyt, Mchezaji wa Liverpool, alimalizia mpira wa Elia aliemhadaa Kipa Sorensen hiyo ikiwa ni dakika ya 85.
Mechi zinazofuata kwa Kundi hili E ni Juni 19 wakati Holland atakapocheza na Japan na Denmark kuivaa Camerou.
Timu:
Holland: 1-Maarten Stekelenburg; 2-Gregory van der Wiel, 3-John Heitinga, 4-Joris Mathijsen, 5-Giovanni van Bronckhorst, 7-Dirk Kuyt, 6-Mark van Bommel, 10-Wesley Sneijder, 8-Nigel de Jong, 23-Rafael van der Vaart, 9-Robin van Persie.
Denmark: 1-Thomas Sorensen; 4-Daniel Agger, 3-Simon Kjaer, 6-Lars Jacobsen, 15-Simon Poulsen, 10-Martin Jorgensen, 2-Christian Poulsen, 20-Thomas Enevoldsen, 12-Thomas Kahlenberg, 19-Dennis Rommedahl, 11-Nicklas Bendtner.
Refa: Stephane Lannoy (France)

No comments:

Powered By Blogger