Thursday 17 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

RATIBA 2010/11 LIGI KUUENGLAND yaanikwa!!
Ratiba ya Msimu mpya wa Ligi Kuu England itakayoanza Agosti 14 leo imetangazwa na Mabingwa Watetezi Chelsea wataanza wakiwa nyumbani Uwanja wa Stamford Bridge kucheza na Timu iliyopanda Daraja West Bromwich Albion.
Timu ya pili Ligi Kuu, Manchester United, wataanza nyumbani Old Trafford kwa kucheza na Newcastle United ambao pia wamepanda Daraja.
Siku hiyo ya ufunguzi, Agosti 14, kutakuwa na Bigi Mechi pale Liverpool watakapoikaribisha Arsenal huko Anfield.
BIGI MECHI:
-Agosti 14: Liverpool v Arsenal
-Septemba 18: Man United v Liverpol
-Oktoba 2: Chelsea v Arsenal
-Desemba 18: Chelsea v Man United.
-Desemba 25: Arsenal v Chelsea
SIKU YA UFUNGUZI Agosti 14:
Aston Villa v West Ham
Blackburn v Everton
Blackpool v Wigan
Bolton v Fulham
Chelsea v West Brom
Liverpool v Arsenal
Man United v Newcastle
Sunderland v Birmingham
Tottenham v Man City
Wolverhampton v Stoke City
Parreira amlaumu Refa kipigo cha Bafana Bafana
Baada ya kufungwa bao 3-0 na Uruguay hapo jana Jumatano Juni 16 na kufanya wawe njia panda kusonga Raundi ya Pili ya Fainali za Kombe la Dunia toka Kundi A, Kocha wa Afrika Kusini Mbrazil Carlos Alberto Parreira amemvaa na Refa Massimo Busacca toka Uswisina kusema : “ Wachezaji wamechukizwa na kila Mtu anasema huyu ndio Refa mbovu kupita wote hapa! Alikuwa akitoa Kadi zisizostahili!”
Refa huyo alimtoa Kipa wa Bafana Bafana, Khune, kwa Kadi Nyekundu na kuipa penalti Uruguay ambayo ilifungwa na Diego Forlan na kuandika bao la pili dakika ya 80.
Bao la kwanza la Uruguay lilifungwa na Forlan dakika ya 24 baada ya kumparaza Mchezaji wa Bafana.
Goli la 3 liliingizwa dakika za majeruhi na Alvaro Pereira.
Afrika Kusini sasa ni lazima washinde mechi yao ya mwisho na Ufaransa ikiwa watataka kufuzu kuingia Raundi ya Pili.
Alhamisi kwenye Kundi hili, Ufaransa inacheza na Mexico.
Timu:
South Africa: Khune, Gaxa, Mokoena, Khumalo, Masilela, Tshabalala, Dikgacoi, Letsholonyane, Modise, Pienaar, Mphela.
Akiba: Josephs, Ngcongca, Sibaya, Davids, Booth, Thwala, Parker, Nomvethe, Moriri, Sangweni, Khuboni, Walters.
Uruguay: Muslera, Maxi Pereira, Lugano, Godin, Fucile, Arevalo Rios, Perez, Pereira, Suarez, Forlan, Cavani.
Akiba: Castillo, Gargano, Victorino, Eguren, Abreu, Gonzalez, Scotti, Alvaro Fernandez, Sebastian Fernandez, Caceres, Silva.
Refa: Massimo Busacca (Switzerland)

No comments:

Powered By Blogger