Wednesday 16 June 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

Ndugu kina Palacios wa Honduras waweka Historia
Honduras imekuwa Nchi ya kwanza katika historia ya Kombe la Dunia kuweza kuwa na Ndugu watatu katika Kikosi chao baada ya kumwita kujiunga na Timu Jerry Palacios kumbadilisha Julio Cesar de Leon alieumia.
Kabla kuitwa kwa Jerry Palacios, Honduras ilikuwa na Kaka zake wawili, Wilson Palacios anaechezea Tottenham na Johnny Palacios wa Olimpia ya huko Honduras.
Jerry Palacios ni Straika toka Klabu ya China Hangzhou Greentown.
Honduras iliruhusiwa kumbadili Mchezaji huyo alieumia kwa vile FIFA inakubali hilo ikiwa tu litafanyika Masaa 24 kabla ya mechi ya kwanza ya Timu.
Familia hiyo ya kina Palacious ilipata balaa Miaka mitatu iliyopita pale mdogo wao Edwin alipotekwa nyara huko Honduras lakini licha ya kulipwa Dola 150,000 ili aachiwe, maiti ya Edwin iliokotwa porini.

No comments:

Powered By Blogger