Monday 14 June 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

Honda ni shujaa Japan!!!!
Bao la dakika ya 39 la Honda limeipiga chini Cameroun kwa bao 1-0 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Free State huko Bloemfontein leo Juni 14 mechi ya Kundi E ambalo awali leo Uholanzi ilishinda 2-0 dhidi ya Denmark.
Kipindi cha pili Cameroun walijitutumua ili warudishe bila mafanikio.
Cameroun inaungana na Algeria na Nigeria kwa kuwa Timu za Afrika zilizofungwa mechi zao za kwanza za Makundi yao kwenye Fainali za Kombe la Dunia.
Timu pakee ya Afrika iliyoshinda ni Ghana iliyoichapa Serbia 1-0 na Afrika Kusini ilitoka sare 1-1 na Mexico.
Nyingine ni Ivory Coast wanaocheza kesho na Ureno.
Mechi inayofuata kwa Cameroun ni Juni 19 dhidi ya Denmark.
Timu:
Cameroon: Hamidou, M'bia Etoundi, N'Koulou, Bassong, Assou-Ekotto, Matip, Makoun, Enoh, Eto'o, Webo, Choupo-Moting.
Akiba: Kameni, Rigobert Song, Alex Song, N'Guemo, Njitap, Emana, Bong, Chedjou, Idrissou, Mandjeck, Ndy Assembe, Aboubakar.
Japan: Kawashima, Nagatomo, Nakazawa, Tanaka, Komano, Matsui,
Honda, Abe, Hasebe, Endo, Okubo.
Akiba: Narazaki, Uchida, Okazaki, Shunsuke Nakamura, Tamada, Yano, Iwamasa, Kengo Nakamura, Konno, Morimoto, Inamoto, Kawaguchi. Referee: Olegario Benquerenca (Portugal)

No comments:

Powered By Blogger