Thursday 8 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Webb wa England kuchezesha Fainali Kombe la Dunia
Refa wa England, Howard Webb, ameteuliwa kuchezesha Fainali ya Kombe la Dunia kati ya Holland na Spain Siku ya Jumapili Julai 11 huko Soccer City, Soweto, Johannesburg.
Mara ya mwisho kwa Refa wa Kiingereza kuchezesha Fainali ya Kombe la Dunia ilikuwa Mwaka 1974 Jack Taylor alipochezesha mechi kati ya Germany v Holland ambayo Germany walitwaa Ubingwa wa Dunia kwa kushinda 2-1.
Refa Howard Webb atasaidiwa na wenzake toka England, Michael Mullarkey na Darren Cann.
Mpaka sasa huko Afrika Kusini, Webb na Timu yake wamechezesha Mechi 3, Spain walipofungwa 1-0 na Uswisi, Slovakia walipoibwaga Italy 3-2 na Brazil kuifunga Chile 3-0.
Katika mechi hizo tatu, Webb hakutoa Kadi Nyekundu wala penalti.
Webb na Wasaidizi wake ndio waliochezesha Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI Mwezi Mei Inter Milan ilipoifunga Bayern Munich 2-0 huko Santiago Bernabeau na kutwaa Ubingwa wa Ulaya.

No comments:

Powered By Blogger