Friday 9 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Brazil yaanua Nembo ya Kombe la Dunia 2014
Brazil, ambao ndio watakuwa Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia Mwaka 2014, leo wameanua rasmi Nembo itayotumika kwenye Mashindano hayo.
Nembo hiyo inayoitwa ‘Msukumo’ [Inspiration] ina mchoro wa Mikono mitatu iliyoshikamana yanye umbo la Kombe la Dunia na una rangi za Kijani na Njano kama Bendera ya Brazil.
Uzinduzi wa Nembo hiyo umefanywa na Rais wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva huko Johannesburg na kuhudhuriwa pia na Wachezaji wa zamani wa Brazil Carlos Alberto, Cafu na Romario pamoja na Kocha wa zamani wa Brazil, Carlos Alberto Parreira, ambae aliifundisha Bafana Bafana kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka huu huko Afrika Kusini.
Rais Lula, katika uzinduzi huo, alisema wana mzigo mkubwa kuyafanya Mashindano ya Mwaka 2014 yawe ya mafanikio kama hayo ya Afrika Kusini.
Lula alitamka: “Mafanikio ya Ndugu zetu wa Afrika ni changamoto kubwa kwa Brazil. Tutajifunza kutoka kwao.”
Nae Rais wa FIFA, Sepp Blatter, amesema Soka huko Brazil ni kama dini na ameisifia kwa kuipa umuhimu kuliko Nchi yeyote.
Brazil ni Mabingwa wa Dunia mara 5 na walikuwa Wenyeji wa Kombe la Dunia Mwaka 1950.

No comments:

Powered By Blogger