Monday 28 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Brazil 3 Chile 0
Ni Brazil v Holland Robo Fainali!!
Brazil wamewatwanga wenzao wa Marekani ya Kusini Chile kwa bao 3-0 na hivyo kuingia Robo Fainali watakayocheza na Holland.
Ni mabao mawili ndani ya dakika 4, dakika ya 34 la Juan na dakika ya 38 la Luis Fabiano, ndio yaliyowalainisha Chile.
Kipindi cha Pili, Robinho alipachika bao la 3 dakika ya 59.
Ulikuwa ni ushindi laini kwa Brazil ambao wanaonyesha wao ni tishio kubwa kwenye Fainali hizi za Kombe la Dunia.
Timu:
Brazil: Julio Cesar, Maicon, Lucio, Juan, Michel Bastos, Ramires, Gilberto Silva, Dani Alves, Kaka, Robinho, Luis Fabiano.
Chile: Claudio Bravo, Mauricio Isla, Pablo Contreras, Ismael Fuentes, Arturo Vidal, Mark Gonzalez, Carlos Carmona, Gonzalo Jara, Humberto Suazo, Jean Beausejour, Alexis Sanchez.
Refa: Howard Webb (England)

No comments:

Powered By Blogger