Sunday 27 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Ghana yajikita Robo Fainali!!
Ghana 2 USA 1
Dakika 120 ziliwaibua Ghana kidedea baada ya Asamoah Gyan kupachika bao la ushindi mara tu baada ya dakika 30 za nyongeza kuanza na kuifanya Afrika nzima ishangilie Ghana kuingia Robo Fainali ya Kombe la Dunia.
Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Royal Bafokeng huko Rustenburg.
Hadi dakika 90, bao zilikuwa 1-1 na ndipo zikaongezwa dakika 30.
Ghana ndio walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 5 Mfungaji akiwa Kevin-Prince Boateng.
Lakini USA walisawazisha Kipindi cha Pili kwa penalti iliyopigwa na Landon Donovan.
Penalti hiyo ilipatikana baada ya Difenda Jonathan Mensah kumwangusha Clint Dempsey ndani ya boksi.
Robo Fainali Ghana watacheza na Uruguay siku ya Ijumaa Julai 2.

No comments:

Powered By Blogger