Saturday 3 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Argentina yasagwa na Mashine ya Kijerumani!!
Germany 4 Argentina 0
Ni wachache mno walioipa Germany nafasi yeyote katika Fainali hizi za Kombe la Dunia lakini baada ya kuibomoa England bao 4-1 leo huko Cape Town Uwanja wa Green Park walishusha kipondo kikubwa kwa Timu ya Maradona, Argentina, iliyokuwa ikisifiwa na wengi kwa kuisaga kwa mabao 4-0 na kutinga Nusu Fainali.
Germany, wakitumia staili ile ile ya kaunta ataki huku Wachezaji wao Viungo wakibadilishana pozisheni kila sekunde kiasi hujui nani anacheza wapi, waliizidi Argentina kwa muda mrefu wa gemu hi na kuwafunika kabisa Masupastaa Lionel Messi, Tevez, Mascherano na wenzao.
Ilichukua dakika 3 kwa Germany kupata bao kupitia Thomas Muller aliefunga kwa kichwa toka frikiki ya Schweinsteiger.
Hadi mapumziko Germany 1 Argentina 0.
Kipindi cha Pili ndipo mashine ya Kijerumani ikapata kasi na kutingisha bao 3.
Bao la pili alifunga Miroslav Klose dakika ya 68 kutoka pasi murua ya Podolski na kumkuta akiwa na nyavu tu mbele yake.
Dakika ya 74 Friedrich akapachika bao la 3 kutoka pande la Schweinsteiger na Klose akapata bao lake la pili na la 4 kwa Germany kwenye dakika ya 88.
Nusu Fainali Germany watacheza na Mshindi kati ya Spain v Paraguay.
Timu:
German: Neuer, Lahm, Mertesacker, Boateng, Friedrich, Schweinsteiger, Khedira, Muller, Ozil, Podolski, Klose.
Akiba: Wiese, Jansen, Aogo, Tasci, Kiessling, Badstuber, Trochowski, Kroos, Cacau, Marin, Butt, Gomez.
Argentina: Romero, Otamendi, Demichelis, Burdisso, Heinze, Maxi, Mascherano, Di Maria, Messi, Higuain, Tevez.
Akiba: Pozo, Rodriguez, Bolatti, Veron, Garce, Samuel, Aguero, Gutierrez, Palermo, Milito, Andujar,
Refa: Ravshan Irmatov (Uzbekistan)

No comments:

Powered By Blogger