Friday 2 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Holland 2 Brazil 1
Brazil wametolewa nje ya Kombe la Dunia kwa kufungwa bao 2-1 na Holland katika mechi ya Robo Fainali ambayo Brazil walipata bao dakika ya 10 tu kupitia Robinho na kuitawala lakini bao 2 toka frikiki na kona yamewapa Uholanzi ushindi katika mechi ambayoWaholanzi  hawakutengeneza hata nafasi moja ya wazi hadi Brazil walipocheza Mtu 10 Felipe Melo alipopewa Kadi Nyekundu.
Uholanzi imetinga Nusu Fainali na Mshindi kati ya Uruguay na Ghana.
Bao la kwanza la Uholanzi lilikuwa la kujifunga wenyewe Felipe Melo alipogonga kwa kichwa mpira na kumchanganya Kipa Cesar.
Bao la pili alifunga Sneijder kwa kichwa kufuatia kona.
Mechi hii ilitawaliwa na uamuzi wenye utata wa Refa Yuichi Nishimura toka Japan akiwaacha Uholanzi wacheze rafu watakavyo na kudanganya waziwazi bila ya kuwapa Kadi na alievunja rekodi ni Van Bommel wa Uholanzi aliecheza kila aina ya rafu na triki na Refa Mjapan akiona ni sawa.

No comments:

Powered By Blogger