Sunday 27 June 2010

TEMBELEA: www.sokainbongo.com

Gyan azawadia ushindi wa Ghana kwa Africa
Asamoah Gyan ametoa zawadi bao lake la ushindi la Ghana ilipoifunga USA 2-1 kwenye dakika 120 za mechi ya Raundi ya Pili jana Jumamosi huko Royal Bafokeng, Rustenburg na kutinga Robo Fainali ambako watacheza na Uruguay Ijumaa Julai 2.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ghana kufika Robo Fainali ya Kombe la Dunia na imekuwa Nchi ya 3 ya Afrika kufika hatua hiyo baada ya Cameroun Mwaka 1990 na Senegal 2002.
Asamoah Gyan, ambae bao lake la dakika ya 93 ndio liliibua mayowe kila kona ya Afrika, ametamka: “Mwaka 2006 tulifika Raundi ya Pili na safari hii tupo Robo Fainali. Hii ni fahari kwa Ghana na Afrika yote!”
Hili ni bao la 3 la Gyan kwenye Kombe la Dunia na limemfanya afungane na Suarez wa Uruguay kama Wafungaji Bora mpaka sasa.

No comments:

Powered By Blogger