Sunday 27 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Luis Fabiano: ‘Man United inavutia!’
-Atangaza kutosaini tena Sevilla!
Straika wa Brazil, Luis Fabiano, Miaka 29, anaecheza Sevilla huko Spain, amedokeza kuwa mara baada ya Kombe la Dunia atahama Klabu hiyo na kusema Manchester United inavutia kwake kwa sababu Kocha wao ni Mshindi na Wachezaji ni Washindi.
Huko Afrika Kusini, Fabiano alipachika bao mbili kwa Brazil kwenye mechi na Ivory Coast waliyoshinda 3-1. 
Fabiano ametamka: “Nishaweka msimamo wangu, siwezi kusaini Sevilla kwani kwa umri wangu lazima nicheze Timu inayowania Mataji makubwa kila wakati. Siwezi kujiunga Tottenham ni afadhali nibaki Sevilla. Uamuzi wangu utakuwa ni Milan au Man United ingawa kucheza pamoja na Rooney ni jambo la kuvutia.”
Luis Fabiano aliongeza kwa kusema Manchester United inamvutia mno kwa vile Msimu baada ya Msimu huwa wanagombea Mataji England na Ulaya na hushinda mara nyingi.
Hivyo, mara baada ya Fainali za Kombe la Dunia atatoa uamuzi wapi atatua.

No comments:

Powered By Blogger