Monday 28 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Argentina nayo….goli la utata!!
Argentina imeifunga Mexico 3-1 na itacheza na Ujerumani Robo Fainali lakini, kama Ujerumani walioifunga England 4-1 na kugubikwa na mzozo wa goli la wazi la England kukataliwa, Argentina nao bao lao la kwanza la dakika ya 26 alilofunga Carlos Tevez lilileta malamiko makubwa toka kwa Wachezaji wa Mexico wakidai Tevez alikuwa ofsaidi kitu ambacho kilikuwa wazi na walimzonga Refa Roberto Rosetti toka Italia wakimtaka aangalie Bigi Skrini ya hapo Uwanjani iliyokuwa ikionyesha marudio ya tukio hilo.
Hata hivyo Refa huyo hakuangalia TV hiyo kwani sheria hazimruhusu.
Mabao mengine ya Argentina yalifungwa na Higuain dakika ya 33 na Tevez tena dakika ya 52.
Bao la Mexico alifunga Mchezaji anaeenda Manchester United, Javier Hernandez ‘Chicharito’ dakika ya 71.

No comments:

Powered By Blogger