Friday 2 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Hodgson ataka Gerrard na Torres wabaki Liverpool
Meneja mpya wa Liverpool Roy Hodgson ana nia ya kuwashawishi Mastaa wakubwa wa Liverpool hasa Nahodha Steven Gerrard na Fernando Torres wabaki Klabuni hapo licha ya kuwepo minong’ono mikubwa wapo njiani kuhama mara baada ya kuondoka Rafael Benitez kama Meneja.
Akiongea na Wanahabari kwa mara ya kwanza tangu athibitishwe kama Meneja mpya wa Liverpool, Roy Hodgson, alisema: “Hii ni Klabu kubwa yenye asili kubwa na kipaumbele kikubwa kwangu ni kuhakikisha Timu inafanya vizuri!”
Hodgson pia alisisitiza kuwa atajitahidi abakishe Wachezaji wote kwenye Timu wakiwemo Mastaa Gerrard na Torres.

No comments:

Powered By Blogger