Wednesday 30 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Nigeria yajitia kibano wenyewe!!
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, ameamrisha Timu ya Taifa ya Nigeria isishiriki michuano ya Kimataifa kwa Miaka miwili kufuatia kutolewa kwenye Kombe la Dunia hatua ya mwanzo ya Makundi huku wakimaliza Kundi lao wakiwa mkiani baada ya kutoka sare na Korea Kusini na kufungwa na Argentina na Ugiriki.
Lakini hatua hiyo ya Serikali ya Nigeria bila shaka itawaletea matatizo makubwa na FIFA ambao hawataki Vyama vya Soka viingiliwe na Serikali na hivi juzi tu waliionya Serikali ya Ufaransa kuhusu hilo.
FIFA wametoa tamko kuhusu Nigeria kwa kusema: “Hatuna taarifa rasmi kuhusu hilo. Lakini, kwa ujumla, msimamo wa FIFA kuhusu kuingiliwa Soka na Wanasiasa unajulikana vizuri.”

No comments:

Powered By Blogger