Wednesday 30 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Brazil wakabiliwa na majeruhi
Ijumaa Brazil wanaivaa Timu ngumu Holland katika Robo Fainali ya Kombe la Dunia huko Uwanja wa Nelson Mandela, Port Elizabeth lakini wanakabiliwa na majeruhi kadhaa kwenye Kikosi chao na pia Mchezaji Ramires kufungiwa baada ya kupata Kadi za Njano mbili kwenye michuano hii na hivyo kulazimika kukosa mechi moja.
Wachezaji majeruhi ni Elano, Felipe Melo na Julio Baptista.
Elano aliumizwa na Cheik Tiote wa Ivory Coast baada ya kutimbwa vibaya kwenye enka.
Nae Felipe Melo pia ana tatizo la enka wakati Baptista ana tatizo la musuli.
WAFUNGAJI BORA KOMBE LA DUNIA:
-Higuain bao 4 [Argentina]
-Villa bao 4 [Spain]
-Vittek bao 4 [Slovakia]
-Donovan bao 3 [USA]
-Gyan bao 3 [Ghana]

No comments:

Powered By Blogger