Wiki mbili Capello kujua hatma yake England!!

Msemaji wa FA amesema hawawezi kutoa uamuzi mara tu baada ya kubwagwa nje ya Kombe la Dunia kwani hilo linaweza kuathiri kutoa uamuzi sahihi na badala yake kutoa uamuzi kwa jazba.
Mwenyewe Capello amesema: “Bado naitaka kazi hii ya England na ndio maana nimekataa kuwa Meneja wa Klabu kubwa kadhaa zinazonitaka.”
Capello aligusia sababu za England kuwa goigoi kwenye Kombe la Dunia na kudai sababu kubwa ni uchovu wa Wachezaji uliosababishwa na kutokuwa na mapumziko majira ya baridi [Desemba na Januari] kama wanavyofanya Nchi nyingine [ikiwemo Ujerumani] ambao Misimu yao huanza Agosti hadi mwishoni mwa Desemba na kupumzika na kisha kuanza tena mwishoni mwa Januari hadi Mei.
England Msimu huanza Agosti hadi Mei mfululizo bila mapumziko.
No comments:
Post a Comment