Monday 9 November 2009

Baada ya mechi ya leo, Ligi Kuu kupisha kitimtim cha Kombe la Dunia hadi Novemba 21!!!
Baada ya mechi ya leo ya Ligi Kuu saa 5 usiku, saa za kibongo, Liverpool kuikaribisha Birmingham Uwanjani Anfield, Ligi Kuu England itakaa pembeni hadi Jumamosi, Novemba 21 ili kupisha mapambano ya kuwania kuingia Fainali za Kombe la Dunia Afrika Kusini 2010 ambayo yatachezwa Jumamosi Novemba 14 na marudiano ni Jumatano, Novemba 18.
Ratiba kuhusu mechi hizo tutawaletea kesho. 
Vilevile, kwa Timu za Taifa ambazo zimefuzu kuingia Fainali hizo za Kombe la Dunia, kipindi hiki ni Kalenda ya FIFA kwa Timu za Taifa kucheza mechi kadhaa za kirafiki na hivyo kuna mechi kadhaa za kirafiki za Timu hizo.
RATIBA YA LIGI KUU NI KAMA IFUATAVYWO:
Jumatatu, 9 Novemba 2009
Liverpool v Birmingham
Jumamosi, 21 Novemba 2009
Birmingham v Fulham
Burnley v Aston Villa
Chelsea v Wolves
Hull City v West Ham
Liverpool v Man City
Man U V Everton
Sunderland v Arsenal
Jumapili, 22 Novemba 2009
Bolton v Blackburn
Stoke v Portsmouth
Tottenham v Wigan
Jumatano, 25 Novemba 2009
Fulham v Blackburn
Hull City v Everton

No comments:

Powered By Blogger