Thursday 12 November 2009

Drogba kujenga Hospitali kwao Abidjan, Ivory Coast!!
Zimeibuka taarifa kuwa Mshambuliaji Nyota wa Chelsea ambae ni raia wa Ivory Coast, Didier Drogba, ameamrisha kitita atakacholipwa na Kampuni ya Pepsi kwa kumtumia ili kujitangaza ambacho ni Pauni Milioni 3 zitumike zote kujenga Hospitali yenye vitanda 200 huko kwao Abidjan, Ivory Coast.
Hospitali hiyo inayotarajiwa kumalizika mwakani 2010 pia itatumika kuwalea watoto yatima.
Mwenyewe Drogba ametamka: “Mwanzoni mwaka huu nilikwenda Hospitali huko Abidjan na nilistushwa kuona hali mbaya mno!! Hapo ndipo nikaamua kujenga Hospitali ili kusaidia watu!”
Yemen 2 Bongo 1
Katika mechi ya pili kwa Yemen na Tanzania huko Sanaa, Yemen, jana Taifa Stars ilifungwa bao 2-1 Uwanjani Ali Mohsin Muraisi.
Mechi ya kwanza Timu hizi zilitoka sare 1-1.
Yemen ndio ilipata bao la kwanza kwa penalti iliyofungwa na Tamer Hanash dakika ya 13 na Bongo wakasawazisha dakika ya 34 kupitia Abdel Halim Mohmad.
Yemen wakapata bao la pili dakika ya 37 Mfungaji akiwa Akram Al-Warafi.

No comments:

Powered By Blogger