Saturday 14 November 2009

New Zealand yaingia Fainali Kombe la Dunia!!
New Zealand 1 Bahrain 0
Leo, ikicheza kwao huko Wellington, New Zealand Uwanja wa Westpac, New Zealand ilifunga bao kupitia Rory Fallon anaecheza Plymouth Argyle huko England dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza na kutinga Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwezi Juni, 2010.
Hata hivyo Bahrain watajuta wenyewe kwani kipindi cha pili walipata penalti na wakakosa kufunga bao ambalo lingewawezesha kuipuku Ne Zealand kwa bao la ugenini.
Katika mechi ya kwanza iliyochezwa huko Bahrain, Timu hizi zilitoka sare 0-0.
Hii ni mara ya kwanza kwa New Zealand kuingia Fainali za Kombe la Dunia tangu mwaka 1982 walipowahi kuzicheza.

No comments:

Powered By Blogger