Thursday 12 November 2009

Ferguson afungiwa mechi 2 na kupigwa Faini!!!
Leo, Kamati ya Sheria ya FA, Chama cha Soka England, kimemtia hatiani Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson kwa kutamka kuwa Refa Alan Wiley hakuwa fiti kuchezesha mpira mara tu baada ya mechi ya Ligi Kuu kati ya Man U na Sunderland iliyomalizika 2-2 hapo Oktoba 3 na kumfungia kutokaa benchi la Timu yake kwa mechi 4 na kulipa Faini ya Pauni Elfu 20 lakini atatumikia kifungo cha mechi 2 tu na mbili nyingine zinasimamishwa ili kuchunga mwenendo wake hadi mwishoni mwa msimu wa 2010/11 na ikiwa hapatikani na kosa jingine adhabu hiyo ya mechi 2 zilizosimamishwa itafutwa.
Ingawa Ferguson aliomba radhi kwa matamshi yake hayo na pia kuomba kwa FA aende mwenyewe kujieleza inaelekea utetezi wake haukufanikiwa. 

No comments:

Powered By Blogger