Sunday 8 November 2009

Chelsea 1 Man U 0
Chelsea mbele pointi 5!!!
Goli la dakika ya 76 alilofunga John Terry [au Anelka aliekuwa ofsaidi huku Drogba akimwangusha Brown!] kufuatia frikiki ambayo Washabiki wa Man U walilalamikia limewapa ushindi Chelsea wakiwa nyumbani Stamford Bridge wa bao 1-0 dhidi ya Mabingwa Manchester United na sasa kuongoza pointi 5 mbele kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Ingawa leo Manchester United walichezesha ukuta dhaifu bila ya Masentahafu wao Nemanja Vidic na Rio Ferdinand ambao ni majeruhi, na ingawa Vidic alikuwa benchi, waliitawala mechi hii na pengine wangeweza kushinda.
VIKOSI:
Chelsea: Cech, Ivanovich, Carvalho, Terry, Cole, Essien, Lampard, Ballack, Deco, Drogba, Anelka.
Akiba: Hilario, Joe Cole, Mikel, Malouda, Paulo Ferreira, Kalou, Alex.
Manchester United: Van der Sar, O'Shea, Brown, Jonathan Evans, Evra, Fletcher, Carrick, Anderson, Valencia, Rooney, Giggs.
Akiba: Kuszczak, Owen, Vidic, Scholes, Fabio Da Silva, Obertan, Gibson.
Refa: Martin Atkinson

No comments:

Powered By Blogger