Saturday 14 November 2009

NGOMA NGUMU!!! Misri 2 Algeria 0, mechi kuchezwa tena Jumatano huko Sudan kupata Mshindi kwenda Kombe la Dunia!!!
Mpaka dakika 90 kugonga, Misri walikuwa mbele bao 1-0 na hivyo wangekuwa nje Kombe la Dunia lakini, makosa ya Algeria ya kujidondosha makusudi ili kupoteza mwelekeo wa mchezo na pia muda, yaliwatokea puani!
Ziliongezwa dakika 6 na ndipo Misri wakapata bao la pili kwenye dakika ya 5 ya hiyo nyongeza na kushinda 2-0.
Lakini ushindi huo umewafanya walingane kila kitu na Algeria na hivyo mechi hiyo itachezwa Uwanja nyutro huko Sudan ili kupata Mshindi atakaetinga Fainali Kombe la Dunia kuungana na Nchi nyingine za Afrika, yaani Afrika Kusini, Ghana, Ivory Coast, Cameroun na Nigeria.

No comments:

Powered By Blogger