Saturday 14 November 2009

Cameroun nao wajikita Fainali Kombe la Dunia
Morocco 0 Cameroun 2
Togo 1 Gabon 0
Cameroun leo wameshinda ugenini huko Morocco na kupata tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani huko Afrika Kusini huku wapinzani wao kutoka KUNDI A waliokuwa wakiwania nafasi hiyo pia, Gabon, kufungwa 1-0 ugenini na Togo.
Mabao ya Cameroun yalifungwa na Pierre Webo dakika ya 18 na Samuel Eto’o dakika ya 52.
Mechi ya Misri na Algeria, inayoanza muda mfupi tu kuanzia sasa, ndiyo itatoa Mwakilishi wa mwisho kutoka Afrika baada ya Timu za Afrika Kusini [Mwenyeji], Ghana [Mshindi KUNDI D], Nigeria [KUNDI B] na Ivory Coast [KUNDI E] kufuzu kuingia Fainali za Kombe la Dunia mapema.

No comments:

Powered By Blogger