Saturday 14 November 2009

Beckham aisaidia LA Galaxy kuingia Fainali ya Ubingwa MLS!!
Kiungo wa England, David Beckham, ametoa mchango mkubwa kwa Klabu yake Los Angeles Galaxy na kuisogeza mbele kuukaribia Ubingwa wa Ligi ya Marekani iitwayo MLS baada ya Timu hiyo kuifunga Houston Dynano 2-0 kwenye Nusu Fainali.
Mabao hayo mawili yalifungwa dakika za nyongeza, dakika ya 104 na 108.
Ni frikiki ya Beckham ndiyo ilimkuta Mfungaji Greg Berhalter na Landon akafunga la pili kwa penalti.
Wiki ijayo, LA Galaxy itacheza Fainali na Chicago Fire au Real Salt Lake mjini Seattle.

No comments:

Powered By Blogger