Tuesday 10 November 2009

Mwana wa Fergie atimuliwa Umeneja Peterborough!!!

Peterborough United, Klabu inayocheza Daraja chini tu ya Ligi Kuu liitwalo Coca Cola Championship, imemwondoa kazini Meneja wao Darren Ferguson [pichani] ambae ni mtoto wa Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson kufuatia matokeo mabaya kwa Klabu hiyo.
Darren Ferguson, umri miaka 37, ndie alieibeba Timu hiyo na kuipandisha Klabu hiyo mfululizo Madaraja mawili juu kutoka LIGI 2 mpaka ilipo sasa kuanzia mwaka 2007.
Lakini msimu huu, kwenye Ligi ya Coca Cola Championship, Timu hiyo imekuwa ikifanya vibaya na Jumamosi ilipigwa 3-1 na Newcastle.
Katika mechi 140 alizokuwa Meneja hapo Peterborough, Darren Ferguson, ameshinda mechi 73 na kufungwa 40 tu.
KOMBE LA DUNIA: Mechi za Lala Salama, Nani kwenda Bondeni?
Tayari Nchi 23 zishapata Tiketi kucheza Fainali za Kombe la Dunia Afrika Kusini 2010, Fainali zitakazoanza Juni 11 na kumalizika Julai 11, na bado kuna nafasi 9 zikidai ili kufanya jumla ya Nchi 32 kwenye Fainali hizo.
LISTI KAMILI YA TIMU 23 ZILIZOINGIA FAINALI NI:
WENYEJI: Afrika Kusini
AFRIKA: Ghana na Ivory Coast [BADO TIMU 3]
ASIA: Australia, Japan, Korea Kaskazini, Korea Kusini
ULAYA: Denmark, England, Germany, Uholanzi, Serbia, Spain, Italy, Slovakia, Uswisi [BADO TIMU 4]
MAREKANI KUSINI: Brazil, Paraguay, Chile, Argentina
MAREKANI KASKAZINI, KATI NA CARIBBEAN: USA, Mexico, Honduras
TIMU ZITAKAZOINGIA FAINALI KUPITIA MECHI ZA MCHUJO [Moja kati ya mbili zifuatazo]:
-New Zealand au Bahrain [Mechi ya kwanza Nchini Bahrain ilikuwa 0-0]
-Costa Rica au Uruguay
-Urusi au Slovenia
-Ufaransa au Republic of Ireland
-Ureno au Bosnia-Herzegovina
-Ukraine au Greece
-AFRIKA [INATEGEMEA MATOKEO KWENYE MAKUNDI YAO]: Wenye matumaini makubwa kupata Nafasi 3 zilizobaki ni:
-KUNDI A- Cameroun au Gabon
Cameroun pointi 10
Gabon pointi 9
Cameroun, ambao watacheza ugenini huko Morocco, wanatakiwa waifunge Morocco ili watinge Fainali.
Gabon ni lazima washinde mechi yao na Togo itakayochezwa huko Togo na pia kuomba Cameroun watoke suluhu au wafungwe.
-KUNDI B- Tunisia au Nigeria
Tunisia pointi 11
Nigeria pointi 9
Tunisia watasafiri hadi Msumbiji na Nigeria watakuwa Kenya kwa mechi zao za mwisho.
Ikiwa Tunisia wataifunga Msumbiji basi watafanikiwa kwenda Fainali.
Lakini hata Tunisia wakitoka sare huko Msumbiji huku Nigeria afungwe au atoke sare na Kenya, Tunisia watapita.
Nigeria ni lazima waifunge Kenya na kuomba Tunisia afungwe au atoke dro.
-KUNDI C- Misri au Algeria
Algeria pointi 13
Misri pointi 10
Ni Misri au Algeria ndio watafika Fainali na Timu hizi zinakutana Mjini Cairo, Misri Jumamosi.
Wakati Algeria inahitaji suluhu tu, au hata wafungwe 1-0 tu, watasonga mbele, Misri ni lazima ishinde kwa goli 3-0 ili wapite.
Mechi ikiisha kwa ushindi wa 2-0 kwa Misri mechi hii inabidi irudiwe Nchi nyutro [si Misri wala Algeria] kwani zitakuwa zimelingana kila kitu.
RATIBA:
Afrika
Novemba 14
Mozambique v Tunisia
Togo v Gabon
Morocco v Cameroun
Rwanda v Zambia
Kenya v Nigeria
Burkina Faso v Malawi
Ivory Coast v Guinea
Egypt v Algeria
Sudan v Benin
Novemba 15
Ghana v Mali
Asia na Oceania
Novemba 14
New Zealand v Bahrain [Mshindi mechi hii ataingia Fainali lakini sare yeyote ya magoli, Bahrain atakuwa Fainali kwa magoli ya ugenini kwani mechi ya kwanza huko Bahrain ilikuwa 0-0] 
Marekani
Novemba 14
Costa Rica v Uruguay
Novemba 18
Uruguay v Costa Rica
Ulaya
Novemba 14
Urusi v Slovenia
Republic of Ireland v Ufaransa
Greece v Ukraine
Ureno v Bosnia-Herzegovina
Novemba 18
Ukraine v Greece
Bosnia-Herzegovina v Ureno
Ufaransa v Republic of Ireland
Slovenia v Urusi
LIVEPOOL 2 BIRMINGHAM 2
Wakiwa nyumbani Anfield, Liverpool jana chupuchupu kufungwa na Birmingham kama si kupewa penalti tata na Refa Peter Walton kwenye dakika ya 71 na Nahodha Steven Gerrard, alieingia toka benchi la akiba, kufunga bao la pili kwa penalti hiyo na kusawazisha.
Penalti hiyo ilikuja baada ya Fowadi wa Liverpool David Ngog kujiangusha bila kuguswa na kumhadaa Refa.
Liverpool walianza kupata bao dakika ya 13 Mfungaji akiwa Ngog na Birmingham wakasawazisha kupitia Benitez dakika ya 26 na Jerome akapachika bao la pili dakika ya 45.
VIKOSI:
Liverpool: Reina, Johnson, Agger, Insua, Skrtel, Riera [Gerrard, dak 45], Benayoun [Babel dak ya 77], Mascherano, Lucas [Aquilani, dak 82], Kuyt, Ngog.
Birmingham: Hart, Carr, Ridgewell, Johnson, Dann, Bowyer, Larsson, Tainio [Carsley, dak ya 15], Jerome, Benitez [McSheffrey, dak ya 86], Mac Fadden [Vignal, dak ya 76]

No comments:

Powered By Blogger