Friday 27 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Wenger ahofia wacheza ‘Raga’ Blackburn!
Jumamosi, Arsenal watatua Ewood Park nyumbani kwa Blackburn Rovers, walio chini ya Meneja Sam Allardyce, maarufu kama Big Sam, na tayari Meneja wa Arsenal ameanza kuigwaya mechi hiyo ya Ligi Kuu kwa kumtaka Refa wa mechi hiyo, Chris Foy, awe makini pengine akiikumbuka mechi ya Msimu uliokwisha walipochapwa 2-1 na Blackburn na Wenger kuulalamikia uchezaji wa nguvu wa Blackburn bila Refa kuwalinda.
Wenger amesema kuwa ni uhuru wa kila Timu kucheza staili wanayoona bora kwao ili mradi inafuata sheria za Soka na Refa anahakikisha sheria za Soka zinafuatwa.
Wenger ametamka: “Timu ikicheza mipira mirefu, ya juu na kutumia ubavu ni sahihi tu lakini wafuate Sheria za Soka na sio kucheza Raga na Refa anatizama tu!”

No comments:

Powered By Blogger