Monday 23 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Fergie kutwangwa Faini?
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, anaweza akakabiliwa na Faini za mfululizo ikiwa hatabadili msimamo wake wa kukataa kuhojiwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC, mara baada ya mechi za Ligi Kuu England kama kanuni mpya za Ligi hiyo zinavyowataka kila Meneja wa Timu awepo kuhojiwa na BBC baada ya mechi za Timu zao.
Ferguson amekuwa na ugomvi na BBC tangu Mwaka 2004 wakati BBC waliporusha kipindi kilichoitwa Baba na Mwana ambacho kilikuwa kinamuelezea Ferguson na Mwanawe Jason ambae wakati huo alikuwa Wakala wa Wachezaji.
Ferguson alidai kipindi hicho kilizungumza upuuzi mtupu na akawataka BBC wamuombe radhi lakini BBC hawakufanya hivyo na yeye tangu wakati huo amegoma kuhojiwa na BBC.
Mara baada ya mechi ya Ligi Kuu hapo jana kati ya Fulham na Manchester United Ferguson alikataa kuhojiwa na BBC.
Kufuatana na kanuni mpya za Ligi Kuu, suala hilo sasa limepelekwa kwenye Bodi ya Ligi Kuu ili lijadiliwe na huenda akatwangwa Faini ya Pauni 1,000.

No comments:

Powered By Blogger