Monday 23 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Blatter awapa matumaini England!
Rais wa FIFA, Sepp Blatter, ametamka itakuwa rahisi kwa Fainali za Kombe la Dunia kufanyika England kwa vile kila kitu kipo yaani Mashabiki, Viwanja na Miundombinu.
Wakati Blatter akiwapa matumaini, Wakaguzi wa FIFA wa Nchi zinazogombea kuwa Wenyeji wa Fainali za Mwaka 2018 na zile za 2022 wametua England kwa ukaguzi wa Maombi ya England ya kuwa Mwenyeji wa Fainali za Mwaka 2018.
Fainali za Kombe hilo Mwaka huu zilifanyika huko Afrika Kusini Mwezi Juni na Julai na Spain kuibuka Bingwa wa Dunia na zile zinazofuata ni Mwaka 2014 na zitafanyika Brazil.
Wakaguzi hao wamekuwa wakitembelea kila Nchi ya muombaji kwa Siku 4.
Ziara hiyo ilianzia Japan, Korea Kusini, Australia na kisha kwa waombaji wa pamoja Uholanzi na Ubelgiji, halafu Urusi na sasa England, na baadae wataendelea kwa waombaji wengine wa pamoja Spain na Ureno, kisha USA na kumalizia Qatar.
Timu hiyo ya Wakaguzi inaongozwa na Rais wa Shirikisho la Soka la huko Chile, Harold Mayne-Nicholls.
FIFA itatoa uamuzi wa nani watakuwa Wenyeji Mwaka 2018 na 2022 baada ya mkutano wao huko Zurich, Uswisi Desemba 2, Mwaka huu.
Hata hivyo, Blatter ameonya Urusi ni Wapinzani wakubwa wa England katika maombi hayo kwani na wao wanazitaka Fainali za Mwaka 2018.

No comments:

Powered By Blogger