Monday 23 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Squillaci kupimwa afya Ze Gunners
Beki kutoka Ufaransa Sebastien Squillaci anategemewa kupimwa afya yake Klabuni Arsenal ili kukamilisha uhamisho wake kutoka Klabu ya Hispania, Sevilla.
Sevilla imethibitisha kuwa Squillaci, Miaka 30, yupo njiani kwenda London kukamilisha taratibu za uhamisho wake.
Arsenal inakabiliwa na uhaba wa Masentahafu baada ya William Gallas, Sol Campbell na Mikael Silvestre kung’oka Klabuni hapo.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ameshamsaini Sentahafu Laurent Koscielny na pia Johan Djourou anategemewa kurudi Uwanjani baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu.
Squillaci alikuwemo kwenye Kikosi cha Ufaransa huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia na alicheza mechi moja.
Mido yupo Ajax
Straika kutoka Misri Mido amehamia Ajax huko Uholanzi kutoka Klabu yake Middlesbrough katika uhamisho wa bure.
Middlesbrough na Mido wamekuwa na mvutano na hatimaye Meneja wa Boro, Gordon Strachan, akaamua kumtema Kikosini na hivyo kumruhusu aondoke kama Mchezaji huru.
Mido, Miaka 27, alianzia kucheza Soka lake huko Ulaya na Ajax na alikaa Miaka miwili na kuondoka Ajax Mwaka 2003 na kuzunguka Klabu kadhaa huko Ulaya zikiwemo Celta Vigo, Marseille, Roma, Tottenham, Wigan, kisha kurudi kwao kuchezea Zamalek na baadae kwenda West Ham.

No comments:

Powered By Blogger