Sunday 22 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Inter yainyuka Roma, yatwaa Supercup
Jana Samuel Eto’o alipachika bao mbili za Kipindi cha Pili na kuiwezesha Inter Milan kuichapa Roma bao 3-1 na kutwaa Supercup Kombe linaloashiria mwanzo wa Msimu mpya.
John Riise ndie alifunga bao kwa Roma lakini Goran Pandev akaisawazishia Inter na kisha Eto’o akapachika mbili na kumpa Meneja mpya wa Inter Milan, Rafa Benitez, Kombe lake la kwanza.
Msimu uliokwisha chini ya Jose Mourinho, aliekwenda Real Madrid, Inter walitwaa Mataji matatu yakiwa ni Ubingwa wa Ulaya, Ubingwa wa Italia na Kombe la Italia.
Barca 4 Sevilla 0
• Yatwaa Spanish Supercup kwa jumla ya bao 5-3
Barcelona, wakiwa kwao Nou Camp, wameweza kuupindua ushindi wa 3-1 wa Sevilla katika mechi ya kwanza na kuichapa Sevilla 4-0 na hivyo kutwaa Supercup kwa jumla ya mabao 5-3.
Lionel Messi wa Barca alipachika mabao matatu na bao pamoja Abdoulay Konko wa Sevilla alijifunga mwenyewe.
Kuyt kwenda Inter Milan?
Straika wa Liverpool kutoka Uholanzi, Dirk Kuyt, ameambiwa na Bodi yao kuwa Inter Milan imetoa ofa ya kumnunua Mchezaji huyo mpiganaji mzuri kiwanjani.
Inter Milan kwa sasa ipo chini ya Meneja wa zamani wa Liverpool, Rafa Benitez, ambae inadaiwa anawataka pia Wachezaji wengine wa Liverpool.
Hata hivyo, Liverpool haijasema nini uamuzi wao kuhusu ofa hiyo ambayo inakadiriwa kuwa Pauni Milioni 15.
Kuyt alijiunga na Liverpool Mwaka 2006 na ni Mchezaji muhimu wa Holland ambayo aliichezea pia kwenye Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na mpaka sasa ameshaichezea Nchi hiyo mechi 70.

No comments:

Powered By Blogger