Friday 27 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

EUROPA LIGI: Droo ya Makundi leo
Baada ya matokeo ya hapo jana kufuatia mechi za marudiano za Raundi ya Mchujo, jumla ya Timu 48 zimepangwa kwenye Makapu Manne kwa ajili ya Droo ya kupanga Makundi.
Kati ya Timu hizo 48, Timu 10 ni zile zilizobwagwa nje ya UEFA CHAMPIONS LIGI kwenye Hatua ya Mchujo ambazo mechi zake za marudio zilichezwa juzi Jumanne na Jumatano.
Droo hiyo itafanyika leo Saa 8, saa za bongo, huko Monaco.
Timu hizo 48 zimepangwa katika Makapu manne, kufuatia Ubora wao, na zitapangwa katika Makundi 12 ya Timu 4 kila moja.
Kila Kapu litatoa Timu moja ili kukamilisha Kundi la Timu 4 na Timu za Nchi moja haziwezi kupangwa Kundi moja.
Timu za Kapu la 1, ambazo ndizo zimepewa Ubora wa juu, ni pamoja na Mabingwa Watetezi wa Kombe hilo, Atletico Madrid na pia wamo Liverpool FC.
Mechi za kwanza za Makundi zitachezwa Septemba 16.
Washindi wawili wa juu wa Kila Kundi watasonga Hatu ya Mtoano ya Timu 32 na idadi hiyo itafikiwa baada ya kujumuika Timu zitakazoshika nafasi ya 3 kutoka Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
MGAWANYO WA MAKAPU:
KAPU LA 1
1 Club Atlético de Madrid (Mabingwa Watetezi)
2 Liverpool FC (England)
3 Sevilla FC (Spain)
4 FC Porto (Ureno)
5 Villarreal CF (Spain)
6 PFC CSKA Moskva (Urusi)
7 PSV Eindhoven (Uholanzi)
8 FC Zenit St. Petersburg (Urusi)
9 Juventus (Italy)
10 Sporting Clube de Portugal (Ureno)
11 VfB Stuttgart (Ujerumani)
12 AZ Alkmaar (Uholanzi)
KAPU LA 2
13 FC Steaua Bucureşti (Roumania)
14 LOSC Lille Métropole (Ufaransa)
15 FC Dynamo Kyiv (Ukraine)
16 RSC Anderlecht (Ubelgiji)
17 Bayer 04 Leverkusen (Ujerumani)
18 Paris Saint-Germain FC (Ufaransa)
19 Club Brugge KV (Ubelgiji)
20 US Città di Palermo (Italia)
21 Getafe CF (Spain)
22 Beşiktaş JK (Uturuki)
23 Manchester City FC (England)
24 UC Sampdoria (Italia)
KAPU LA 3
25 AC Sparta Praha (Czech)
26 AEK Athens FC (Ugiriki)
27 FC Metalist Kharkiv (Ukraine)
28 PFC Levski Sofia (Bulgaria)
29 Rosenborg BK (Norway)
30 FC Salzburg (Austria)
31 PFC CSKA Sofia (Bulgaria)
32 Odense BK (Denmark)
33 SSC Napoli (Italia)
34 BV Borussia Dortmund (Ujerumani)
35 NK Dinamo Zagreb (Croatia)
36 FC BATE Borisov (Belarus)
KAPU LA 4
37 Aris Thessaloniki FC (Ugiriki)
38 SK Rapid Wien (Austria)
39 PAOK FC (Ugiriki)
40 KKS Lech Poznań (Poland)
41 FC Karpaty Lviv (Ukrania)
42 BSC Young Boys (Uswisi)
43 FC Utrecht (Uholanzi)
44 KAA Gent (Ubelgiji)
45 FC Lausanne-Sport (Uswisi)
46 FC Sheriff (Moldova)
47 Debreceni VSC (Hungary)
48 HNK Hajduk Split (Croatia)

No comments:

Powered By Blogger