Wednesday 25 August 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

Gerrard na Torres kuikosa Ulaya kesho!
Liverpool wamesafiri hadi Uturuki kwa ajili ya Mechi ya Marudiano ya EUROPA LIGI na Trabzonspor bila ya Mastaa wao wakubwa Nahodha Steven Gerrard na Fernando Torres.
Liverpool walishinda mechi ya kwanza nyumbani Anfield kwa bao 1-0.
Gerrard inasemekana anaumwa mgongo na Torres amepumzishwa na Meneja Roy Hodgson ili kumnusuru kucheza Mechi tatu mfululizo hasa ukizingatia matatizo yake ya kuumia mara kwa mara yaliyokuwa yakimkumba.
Nae Javier Mascherano pia hayumo kwenye msafara huku habari za kuhamia kwake FC Barcelona zikipeperushwa angani.

No comments:

Powered By Blogger