Thursday 26 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

WACHEZAJI BORA WA MWAKA UEFA watajwa: Wachezaji wa Mabingwa Inter Milan wakwapua zawadi zote 5!!!
• Diego Milito MCHEZAJI BORA ULAYA!!!
Sambamba na kupangwa kwa Droo ya Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI, pia kulikuwa na kinyang’anyiro cha Tuzo za Wachezaji Bora wa Ulaya kwa Msimu wa 2009/10 na Wachezaji wa Mabingwa wa Ulaya Inter Milan ndio walionyakuwa Tuzo zote 5.
Diego Milito ndio aliibuka Mchezaji Bora wa Mwaka pamoja na kutwaa pia Tuzo ya Straika Bora wa Mwaka.
Diego Milito, atokae Argentina, ndie alifunga bao zote mbili zilizoiua FC Barcelona kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI na kuipa Inter Milan Ubingwa.
MCHEZAJI BORA: Diego Milito (Inter Milan)
KIPA BORA: Julio Cesar (Inter Milan)
DIFENDA BORA: Maicon (Inter Milan)
KIUNGO BORA: Wesley Sneijder (Inter Milan)
FOWADI BORA: Diego Milito [Inter Milan]

No comments:

Powered By Blogger